NENO LA LEO: ZABURI 119:9
“Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako”
TAFAKARI:
Katika kizazi chetu, tunashuhudia waganga wa kienyeji wakipata umaarufu wa kupata wateja wengi, na moja ya tiba wanayotoa ni KUSAFISHA NYOTA, hii ina manisha kuondoa Mikosi, Nuksi n.k.
Dada mmoja alitoa ushuhuda wa mambo aliyofanyiwa na Fundi (Mganga wa Kienyeji) alipoenda kusafisha nyota ya Mapenzi – Tatizo lake lilikuwa kila akimpata Mwanaume anaishia kumtimizia haja ya Mwili baadaye anaachwa. Katika tiba ya kusafisha Nyota alifanyiwa Mambo ya aibu, ikiwemo kuchanjwa chale sehemu zake za Siri na kulazimika kufanya Ngono na huyo fundi ikiwa ni sehemu ya Tiba. Pamoja na yote hayo hakufanikiwa, mpaka alipojisalimisha Kwa Mungu. Hadi sasa baada ya maombi, Yule Dada ana Mume na watoto Ndani ya YESU.
Vijana wengi, wanahangaika kwa kukosa elimu ya Mungu, wanajiingiza katika mitindo ya maisha inayowatenga na Mungu wao, na mwishowe wanaishia kukata tamaa. Leo nahitaji kujibu baadhi ya Maswali niliyoulizwa na Vijana katika mfululizo wa masomo ninayotoa.
Swali: Je ni halali kuwa na wachumba zaidi ya Mmoja?
Jibu: Hapa kuna shida, huenda hata maana ya uchumba haieleweki, mchumba ni Yule ambaye tayari mmekubaliana na amekubalika na wazazi. Mahusiano mengine nje ya hayo sio uchumba. Mchumba ni mmoja tu, ni udanganyifu kuwa na wachumba wengi. Ukimtegemea Mungu atakupatia Mmoja anayefaa, kuliko kujiingiza katika mtego wa kumkubali kila anayeonekana, mwisho ya yote ni kujichanganya na wote kutoweka.
Swali: Nina Mchumba anataka TENDO la Ndoa kwanza kabla ya kuoana.
Jibu: Kama neno lilivyo, TENDO la NDOA ni kwa walio oana tu, ndiyo maana hakuna TENDO la UCHUMBA. Kitendo hicho nje ya Ndoa ni UZINIFU. Na Amri ya saba inasema “USIZINI” Kutoka 20:14. Athari za kufanya Ngono kabla ya Ndoa ni nyingi sana, Siku zijazo nitakuwa na mada hiyo tu. Matatizo katika ndoa za siku hizi asilimia kubwa yanatokana na Tendo la Ngono kabla ya Ndoa.
Swali: Muda unaenda Siolewi! Nifanyeje?
Jibu: Kuna sababu nyingi zinazosababisha mabinti wasiolewe, zikiwemo maisha aliyoyapitia huko Nyuma, kukataa wachumba katika muda muafaka n.k. pamoja na sababu zozote zile – Ukimtemea Mungu 100%, ninakuhakikishia kuwa Utaolewa. Jumapili ijayo tunapokea mahali ya Dada mwenye Umri wa Miaka 47 anaolewa na mwanaume wa miaka 48. Wote hawajawahi kuoa au kuolewa. Huwezi amini, lakini ndivyo. KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA, BILA KUJALI YA NYUMA, TOA MAISHA YAKO KWA MUNGU NAYE ATAJIBU KWA WAKATI.
Swali: Sioni mwanamke wa Kuoa, nifanyeje?
Jibu: Wanawake wapo, ila huwaoni kwa sababu unatumia vipimo vya kibinadamu. Mwambie Mungu atakuletea Mwenzi wa kukufaa kwa Vipimo vya Mbinguni. Tatizo kubwa, Vijana wa kiume wanatawaliwa na TAMAA za ngono, hivyo wana ONJA ONJA na mwishowe wanaona wanawake wote walishaonjwa. Jambo la kushangaza ni hili – Wanadai mabinti sio waaminifu wakati wao wenyewe ndiyo wamewafikisha katika hali hiyo. Inakuwaje Mtu asiyemwaminifu anatafuta kuishi ni Mtu Mwaminifu? Huko ni kujichanganya.
USHAURI: Vinaja wa kiume na wa kike, wote mnafaa kuoa na kuolewa, ili mradi mmekubali kuzisafisha njia zenu. Tuna shuhudia Kahaba akimpokea Yesu baadaye anakuwa Mama wakufaa, mfano ni Mariam Magdalena alikuwa kahaba – alipokutana na Yesu pale kisimani – Alibadilika akawa kati ya wanawake waadilifu na BORA, waliofaidi mibaraka ya Mungu.
VIJANA MUNGU AWABARIKI – AWAPATIE MAISHA MEMA
Na: Eliezer Mwangosi
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
ReplyDeleteMume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159 dawnacuna314@gmail.com